Mhaga: Lolote atakalowaambieni, Fanyeni!
Lolote atakalowaambieni,
fanyeni! (2:1-12)
Utangulizi
Yesu, Maria na Kanisa
Lake
Katika harusi ya Kana ya Galilaya—Mama Maria yupo. Lakini na Yesu na
wanafunzi wake walialikwa. Hapo, ishara ya kwanza itatendeka kwa ombezi la Mama
Maria. Lakini tujiulize maswali matatu:
b)
Mbona ni Maria tu
anayetambua hilo hitaji? Bila kuombwa tena.
c)
Bila Yesu na Maria
ingekuwaje harusi ya Kana?
Maria ni Jicho la Mungu
Kwanza, kulingana na mapokea Maria alijiimarisha sana katika upendo wa
jirani. Labda umaarifu wake unatokana na kuwa Mama wa “Mwalimu Yesu”. Lakini
mbona “Msema Chochote” haoni hitaji—alipaswa kuliona kwa sababu ni jukumu
lake—lakini Maria asiyehusika ndiye anayeliona? Tuone kwamba Maria hakualikwa, lakini alikuwepo! Kadiri ya
Zaburi 139, Mungu anajua maisha (yakiwemo mahitaji, mapungufu) yetu hata kabla
ya kutuumba. Moyo wa Maria “uliliona hitaji” la Elizabeti (mama wa Yohane
Mbatizaji) bila kuitwa au kualikwa, akaenda kumhudumia kwa miezi mitatu. Kifupi
nafikiri kuwa Maria ni jicho la Mungu, la
kuonea mahitaji yetu hata yale tusipokwalika au kumwomba.
Mungu aliyeyaona mateso ya Waisraeli waliokuwa utumwani Misri (Kut. 3:7).
Sasa anamtumia Maria kama jicho lake la kuonea mahitaji ya watu! Lakini tuelewe
kwamba moyo wa Maria wenye hisi ya Mungu ndilo jicho la Mungu.
Maria anakuwa kiungo, njia, daraja kati ya Mungu (Yesu) na wanaharusi
(waamini wote). Ndio maana Maria anaonana kutoa mwelekeo, agizo kwa wahudumu:
“Fanyeni lolote atakalowaambia” (Yoh. 2:5). Katika haya ya 7, Yesu anawaagiza,
“Jalizeni mabalasi haya maji”. Waliyajaza furi. Yalikuwa sita. Agizo la pili,
“Choteni mmpelekee mkuu wa meza.” Kumbe maji yalishageuka kuwa divai—tena bora
kuliko ile iliyotengenezwa na maharusi!
Fadhila ya Utii
Hilo limetendeka kwa sababu wahudumu wametii agizo la Yesu! Petro na
wenzake walivua bila kuambulia chochote (Luka 5:4). Tupa jarife katika kina cha
ziwa na utapata: walipata samaki 153!
Kutindikiwa divai kwa wanaharusi kunakuwa uwanja wa kutendea muujiza! Ina
maana Mungu alipotuumba tuna vikomo, dhambi ya asili, madhaifu na juu ya yote
kutindikiwa wokovu, aliandaa jukwaa la kututendea miujiza. Na kama Musa
alishika nafasi ya mshenga mkuu—Yesu amejitwalia Ushenga Pekee!
Nipo katika Historia ya Wokovu
Maria ananijua na anakujua. Anajua tunachotindikiwa. Hiyo ndiyo divai yako.
Kama divai ni kileta furaha katika harusi, wewe nawe unachotindikiwa ni kileta
furaha katika maisha yako.
Lakini agizo la Maria, “fanyeni kila atakalowaambieni”, kutimizwa kwa agizo
hilo kulileta muujiza.
Mungu humwambia kila mmoja wetu:
a)
Tubu na uiamini injili
(Yesu) -
b)
Omba na utapewa, bisha
hodi utafunguliwa, tafuta utaona -
c)
Unapenda kunifuata?
Jikane mwenyewe, chukua msalaba wako kila siku, nifuate -
Tunajua kuwa Mungu alimwagiza baba yetu na mama yetu, Adamu na Eva
wakakaidi—wakajipotezea na kutupotezea wokovu. Sasa Maria ndiye Eva mpya.
Anatufundisha kwa maisha, uamuzi na utekelezaji wake jinsi ya Mungu kufanya
muujiza mkuu kuliko yote: kumruhusu Mungu kugeuka kuwa mwanadamu (na bado
anabaki kuwa Mungu).
Tushike agizo lake Maria. Fanyeni lolote atakalowaambia.
Tunaweza kutimiza mambo kadhaa aliyotuagiza Yesu:
yohane 15:7... “Ukiungana nami na maneno yangu yakikaa ndani yenu, ombeni
lolote mtakalo na mtafanyiwa. Hila lina maana: Kukaa katika hali ya neema na
kuomba chochote!

Pd. Philip Ntonja, SSC
15 Machi 2017
Mhaga
Comments
Post a Comment
Thank you for visiting Bits of the Gospel. We appreciate your comments and support.