TYCS - Muungano wa Mt. Cottolengo (MOCK)



Muungano wa Mt. Joseph Benedict Cottolengo

(TYCS – Minaki, Overland, Chanzige, na Kimani)
s.l.p. 28017 kisarawe - pwani

1.       Jina

Jina rasmi la Muungano Muungano wa Mt. Joseph Benedict Cottolengo. Kifupi cha jina la Muungano ni Herufi za Kwanza za Matawi Husika. (MOCK – Minaki, Overland, Chanzige, na Kimani).

2.      Historia

TYCS ni umoja wa wanafunzi wakatoliki Ulimwenguni. Inajulikana kama vijana wanafunzi wakikristu. Hili kutimiza lengo la “kumleta Kristu katika mazingira ya Mwanafunzi”, na kuwasaidia Vijana Wakatoliki kujiamini zaidi katika kuishi maisha yao shuleni, ushirika huu wa kitume unaendelea kutafuta mbinu zaidi za kuboresha mikakati yake. Moja ya mbinu hizo ni kuunda Kanda na Muungano, ambayo huleta matawi zaidi pamoja hili kuwapa huduma za kiroho kwa urahisi na ufanisi.

Muungano wa Mt. Joseph Benedict Cottolengo ulianzishwa mwaka 2010, ukileta pamoja matawi ya Minaki Sekondari na Chanzige Sekondari, kwa wakati huo ukiitwa MICHA. Wakitambua kwamba YCS ni njia nyoofu ya kuwasaidia vijana kuishi imani yao vyema zaidi, Walezi na Viongozi wa matawi haya mawili, chini ya Ofisi ya Vijana ya Parokia ya Mt. Stefano Shahidi, Kisarawe, waliweka misingi ya Muungano huu kwa kuteua viongozi wa Kwanza wa Muda.

Mafanikio mengi yalipatikana kwa kuwaleta pamoja vijana wa matawi haya mawili mara kwa mara. Misa za Pamoja (Joint Mass), Kuwatembelea maskini (Matendo ya Huruma), Kuunda kwaya ya Muungano wakishirikiana na Umoja wa Vijana Parokia, semina za pamoja, na mafungo ni baadhi ya matukio yaliyodhihirisha mshikamano huo kuinua ushiriki katika matawi husika.

Mwaka 2012, baada ya juhudi za kufungua matawi ya Sekondari za Kimani na Overland, Viongozi wa Muungano pamoja na Walezi waliazimia kuupanua Muungano hili kuyashirikisha Matawi hayo mawili. Ni katika zoezi la pamoja la Kuamua hatma ya Muungano ambapo Viongozi wote na Walezi walikubaliana kubadilisha Muungano wa Mt. Joseph Benedict Cottolengo (MICHA) kuwa MOCK.

Tarehe 26/05/2012 iliweka kuwa siku ya kuzindua Muungano huu wa MOCK. Katika shughuli ile, Vijana wa Matawi ya Minaki, Chanzige na Kimani walishiriki kwa Wingi. Walikuwa takriban 120, pamoja na baadhi ya walezi. Kaulimbiu ya siku ilikuwa, “Kijana Mkatoliki na Imani”. Tawi la Overland alikuweza kushiriki kwa sababu ya umbali.

Katika tukio la pili la Muungano, matawi yote ya MOCK yalishiriki na hivyo kutimiza ndoto za wanzilishi wa Muungano huu. Tarehe hiyo ya 30/09/2012, palikuwa na Misa ya Pamoja, ambapo Kwaya ya Muungano iliongoza kwa nyimbo. Walezi wa matawi yote walishiriki na vijana nao waliweza kukaa pamoja na kubadilishana mawazo.

3.      Dhima

Lengo kuu la Muungano wa Mt. Joseph Benedict Cottolengo ni kuwaleta vijana wakatoliki pamoja katika urika unaowapa nafasi ya kukua pamoja na kuelimishana chini ya walezi, kwa mfano wa Mt. Joseph Benedict Cottolengo.

4.      Dhamira

Muungano unatazamia kuwa Chachu ya maendeleo ya kiroho kwa vijana wa Sekondari zote (na Vyuo) vya Kisarawe, kwa kuupeleka upendo wa Mungu Baba Mpaji kwa wahitaji wa kila aina nje na ndani ya Muungano.

5.      Tunu na Fadhila

Muungano huu unaongozwa na tunu bora za maisha ya Kikristu alizofundisha Mt. Joseph Benedict Cottolengo: Imani kwa Mungu Mpaji, Upendo kwa Maskini Ndugu zetu, Matumaini makuu yaliyojengwa juu ya Upendo wa Mungu kwetu.

Vijana wanajituma kuishi tangu sasa fadhila zote alizoishi kwa njia ya pekee Mt. Joseph Benedict Cottolengo, yaani, Upendo wa dhati haswa kwa maskini, uadilifu, bidii katika maisha, utulivu, furaha, na uchaji.

6.      Kaulimbiu

Kaulimbiu ya Muungano ni “Upendo wa Kristu unatumiliki” – Caritas Christi Urget Nos! (2 Kor 5:14).

7.      Nembo

Alama yetu ya wazi vijana walikusanyika chini ya Msalaba, ikiashiria kwamba Vijana wanatambua Msalaba kama alama ya Ukombozi, kuitetea bila aibu, na kuishi kulingana na mafundisho ya kanisa. Nembo hii inaweza kubadilishwa au kuongezwa vipengele vinavyoonyesha lengo kuu la Muungano.

8.      Uanachama

Kama chama cha Wakristu wakatoliki kinachowaleta vijana pamoja kwa nia ya kuchangia katika malezi yao ya kiroho, kijamii, kiakili, na kibinadamu, mwanachama lazima atimize vigezo vifuatavyo:

1.      Awe Mwanachama hai wa mojawapo wa Matawi yanayounda Muungano wa Mt. Joseph Benedict Cottolengo.

2.      Atimize vigezo vilivyowekwa kwa uanachama wa TYCS, kulingana na Mwongozo wa YCS.

3.      Atimize vigezo vinginevyo vinavyowekwa kupitia vikao halali vya Muungano vilivyoidhinishwa na Walezi.

 

9.      Uongozi

 Tunatambua uongozi kama karama tunayopewa na Mungu na hivyo viongozi wetu ni chachu ya kujituma katika kila jambo jema. Muundo wa Uongozi ni ule ulioidhinishwa na TYCS kitaifa. Kwa kipengele hili, tunatumia “Kitabu cha Kujiongoza.”

10.   Itimisho

Somo wetu Mt. Joseph Benedict Cottolengo awe mfano na mwombezi katika kutimiza. Alipokea ujumbe wa Kristu: “Tafuteni Kwanza Ufalme wa Mbinguni na mengine yote mtayapata kwa ziada.” (Mt. 6:33). Lengo letu basi liwe kutanguliza Ufalme wa Mbinguni hili mengine yote yawe Baraka kwetu.

Comments

Popular posts from this blog

Mwana Mpotevu au Waana Wapotevu?