Jubilee ya Miaka 100 ya Upadre Tanzania
Jubilee ya Miaka 100 ya Upadre Tanzania
SALA YA KUWAOMBEA MAPADRE
Yesu
mpendelevu, uangalie kwa mapendo kazi na mateso ya Mapadri wako; ubariki na
ustawishe mafundisho yao; wanapowafundisha watoto, wanapowahubiria watu,
wanapowatuliza wakosefu watubu na wanapowasaidia wagonjwa na wale wanaokaribia
mauti, Ee Yesu uwe pamoja nao. Uwakinge na hatari zote za roho na za mwili.
Mwokozi
Yesu, ulijalie Kanisa liwe na Mapadri wengi walio Watakatifu. Uwajalie watoto
na vijana wengi wasikie wito wa Upadri, uwatie furaha na Utakatifu na roho za
Mapadri waliokufa uzijalie pumziko la amani.
Kwa mimi mwenyewe Ee Yesu mpendelevu,
naomba unijalie roho ya imani na utii mnyenyekevu ili niwaheshimu Mapadri kama
Mawakili wa Mungu. Niwatii katika njia zote za wokovu wa roho yangu. Amina.
Comments
Post a Comment
Thank you for visiting Bits of the Gospel. We appreciate your comments and support.