Uongozi wa Vijana, 2013-2015

Uchaguzi uliofanyika Dominika ya Epifania, tarehe 06/01/2013, katika ukumbi wa parokia ulidhihirisha ukomavu wa vijana wa Kisarawe, ambapo waliwachagua viongozi wao kwa miaka mitatu ijayo.
Hata kama viongozi watatu kati ya watano waliochaguliwa walishakuwa katika kamati Tendaji, walishika nafasi tofauti. Aliyekuwa Katibu alichaguliwa kuwa Mwenyekiti mpya naye alikuwa Mwenyekuwa akachukua nafasi ya Katibu. Aliyekuwa Katibu Msaidizi alichaguliwa kuwa Mhazini mpya. Makamu Mwenyekiti  na Katibu Msaidizi ni wapya katika kamati hii.

Tunawapongeza Vijana wa Parokia hii kwa kuchagua viongozi wanaoaminika. Tuwaombee Vijana waendeleze ushirikiano huu na kuimarisha zaidi na zaidi utume kwa vijana. Tunawashukuru na kuwapongeza viongozi wapya kwa kukubali kuchukua uongozi na kuuendeleza kulingana na mapokeo ya Kanisa Katoliki. 
Mwaka huu wa Imani, uwe nafasi kwetu kuishi kikamilifu wito wetu kama Vijana wakatoliki.

  Umoja wa Vijana
Parokia ya Mt. Stefano Shahidi Kisarawe

Viongozi wa Vijana


Mwenyekiti: Nd. Veronica Kavishe

M/Mwenyekiti: Nd. Matthias Kazonda

Katibu: Nd. Gernana Mchilla

Katibu Msaidizi: Nd. Stanley Haron

Mhazini: Nd. Alphonse Majugana

 

  Walezi:
Sr. Maria Cesaria
Sr. Hellen Murungi
Fr. Nicholas Kirimo

Comments

  1. mwenyezi mungu atutangulie katika kuhubiri na kuitangaza injili , umoja na ushirikiano miongoni mwetu ndio kiongozai mkubwa aliye juu yetu.

    ReplyDelete

Post a Comment

Thank you for visiting Bits of the Gospel. We appreciate your comments and support.

Popular posts from this blog

TYCS - Muungano wa Mt. Cottolengo (MOCK)

Mwana Mpotevu au Waana Wapotevu?