JE, UNAICHUKULIAJE BIBLIA?



Je, unaichukuliaje Biblia?

Kwa maoni yako …

- ni tunda la busara za mwanadamu?
- ni kitambu cha hadithi na nahau?
- ni Neno la Mungu?

Biblia inasemaje?
“Maandiko matakatifu yote ni uvuvio kutoka kwa Mungu.” (2 Timotheo 3:16)

Ina maana hii kwako:
- majibu ya kuridhisha juu ya mambo makubwa ya maisha (Methali 2:15).
- misingi dhabiti ya maisha ya kila siku (Zaburi 119:105).
- matumaini halisi ya maisha ya baadaye (Warumi 15:4)

TUNAWEZA KUAMINI INACHOSEMA BIBLIA?
Ndio, angalau kwa sababu tatu:
ü      Mwendelezo wa ajabu
Biblia imeandikwa ndani ya miaka 1600 na watu kama arobaini hivi. Wengi wao hawajulikani kamwe.
ü      Uwazi katika kueleza historia.
Wanahistoria kawaida hujaribu kuficha kushindwa kwa watu wao. Baadala yake, waandishi wa Biblia wanaripoti kila kitu bila kuficha mapungufu yao na ya taifa yao. (2 Nyakati 36:15, 16: Zaburi 51:1-14)
ü      Kutimia kwa unabii
Biblia ilitabiri kuanguka kwa mji wa Babilonia karibia miaka 200 kabla ya kutokea kwake (Isaia 13:17-22). Ilieleza sio tu jinsi mji huu ungeanguka bali pia jina la yule aliyeuteka (Isaia 45:1-3).
Mambo mengine mengi yaliyoandikwa yametimia. Je, nasi tutarajie nini kutoka kwa Mungu? (2 Petro 1:21)


Comments

Popular posts from this blog

TYCS - Muungano wa Mt. Cottolengo (MOCK)

Mwana Mpotevu au Waana Wapotevu?