Posts

Showing posts from July, 2015

Kama unajua...

Image
Kama unajua... Utangulizi Mara kwa mara katika malezi ya watoto na vijana, wazazi na walezi ulalamika sana wakisema vijana wao hawataki kutii tena. Kwa upande wao, watoto na vijana (hasa vijana), wanalalamika kwamba wazazi wao hawawaelewi na wanawanyima uhuru wao. Ukihoji vijana uhuru ni nini, mara nyingi wanajidai kueleza uhuru kuwa ni "nafasi ya kufanya kila mmoja atakavyo!" Na wazazi na walezi kwa pamoja wanapingana na mtazamo huu. Bila shaka, kutaka kutenda bila kujali matokeo yake ni ujinga. Ni kama boti kuacha usukumwe na upepo bila mwelekeo. Inahitaji mwelekezi! Uhuru ni nini? Hekima za milenia za Kanisa Katoliki Jibu la swali hili lipo katika Katekisimu ya Kanisa Katoliki (KKK. 1731). "Uhuru ni nguvu ndani ya mtu ya kukua na kukomaa katika ukweli na wema. Uhuru upata ukamilifu wake unapoelekezwa kwa Mungu, heri yetu." Mizizi ya uhuru ipo katika akili na utashi. Hivyo, ni uwezo wa kutenda au kutotenda, kufanya hiki au kile, kutenda matendo yake mwe

Je, Unajua?

Image
Je, unajua? Katika kusafiri, mara kwa mara unasikia watu wakiongea kuhusu maswala ya imani katika daladala. Wanabishana na kugombana kuhusu mambo ambayo wanadhani ni muhimu kuyasimamia hata kwa "hasira". Hivi, umeshajiuliza kama kuingia katika uzima wa milele (mbinguni) ni matokeo ya nini? Mimi nimejiuliza mara nyingi tu baada ya kumsikia bwana mmoja akimkemea mwenzake hadharani (katika mabasi ya kwenda mikoani), kwamba asipojituma zaidi katika "kumfurahisha Mungu" ataenenda zake jehanamu ya moto! Busara za Mafundisho ya Kanisa Katoliki Jibu lipo katika Katekisimu ya Kanisa Katoliki: "Heri ya uzima wa milele ni paji la Mungu tu; ni paji la kimungu kama ilivyo neema inayoelekeza huko." (KKK. 1726) Neema ni kipaji cha Mungu tunachopewa ili tuweze kufika mbinguni! Basi, kumbe kuingia mbinguni ni kwa neema tu. Hata kujituma hili uingie mbinguni ni swala la neema tu. kazi ipo hapa: katika kutambua umuhimu wa neema hiyo kutoka kwa Mungu, kuiomba, kuit