Posts

Showing posts from May, 2013

Kanda ya Mt. Aloyce, Pugu: Tawi la Kimani

Ufunguzi wa Tawi la Kimani Secondary School – Kisarawe Kanda ya Mt. Aloyce – Pugu                            Friday, May 10, 2013 _____________________________________________________ Utangulizi Kwa mkusanyiko huu wa watu, kwa maandalizi haya ya kipekee kabisa, kwa Ibada hii ya Misa Takatifu, tunazindua rasmi tawi la TYCS Kimani, Kanda ya Mt. Aloyce Pugu. Ni tendo la imani. Na kwetu vijana wakatoliki, ikizingatiwa kuwa huu ni Mwaka wa Imani, sina shaka kabisa tendo hili linatuimarisha zaidi kiroho. Kama TYCS ni chama cha Kitume kinachowaleta pamoja Vijana Wakatoliki wa Shule za sekondari hili kumleta Kristo katika mazingira ya shule, ni wazi kabisa kwamba leo, kwa njia ya Pekee, Kristo anakuja katika mazingira ya shule ya Kimani (Wilaya ya Kisarawe). Yesu anakuja sio kuingilia programu za shule au kuvuruga amani yetu kama wanafunzi bali kutuimarisha katika shughuli nyeti iliyotuleta hapa Kimani Sekondari. Ni katika kufuata maadili na mafundisho ya kijana mkatoliki un

Tutafakari Maisha yake

Image
Hand drawing-St. J B Cottolengo by Kirimo "Kwani wote wanaoongozwa na Roho wa Mungu ni wana wa Mungu, kwa maana hamkupata roho ya utumwa mwogope tena, bali mmepokea Roho anayewafanya kuwa wana wa Mungu na kuita, "Abba! Baba!" Roho mwenyewe hushuhudia roho zetu ya kuwa sisi  ni wana, tu warithi pia, yaani warithi wa Mungu wanaorithi pamoja na Kristo, tukiwa tunavumilia mateso pamoja na Kristu, tupate kutukuzwa pamoja naye." (Rom. 8:14-17) Ni dhahiri kabisa kwamba Mt. Joseph Benedict Cottolengo sio tu mwana wa Mungu bali mwana Mpendwa na Mpenda Mungu. Upendo huu wa pekee kwa Mungu ulitokana na imani yake dhabiti. Kama Kijana alielimika katika mafundisho makuu ya imani. Alijua kuwa Mungu ametupa wote upendeleo wa pekee sana, ambapo kila mmoja wetu alipewa nafasi ya pekee machoni pa Mungu. Kwanza kabisa, imani hii ilimjengea msimamo na tabia ya aina yake. Katika utendaji kazi wake kama padre, alijitahidi kuwa na upendo wa pekee kwa kila mmoja, akiwapa nafasi ya